Thursday, February 6, 2014

WATU ZAIDI YA 8 KUNUSURIKA KIFO WAKIWA CHINI YA MGODI HUKO JOHANNESBURG


mgodiMoto ulizuka katika mgodi siku ya Jumanne umbali wa mita 1,700 chini ya ardhi na kusababisha vipande vya mgodi huo kudondoka na kuwaangukia wafanyakazi waliokua kazini siku hiyo.
Hadi sasa waokoaji wamepata miili 8 kutoka ndani ya mgodi huo na bado kuna mfanyakazi mmoja hajapatikana kutoka kwenye huo mgodi wa Doornkop ambao upo Magharibi mwa Johannesburg.
Wachimbaji nane walipatikana wakiwa hai katika chumba kimoja chini ya ardhi ambako walijificha ili kuepuka hayo mawe na moto ambao hadi sasa chanzo chake hakijajulikana.