NLC

Friday, June 21, 2013
BREAKING NEWSSSSS MEYA AFYATULIWA RISASI
Meya wa mji mkuu wa Uganda,Kampala amesema amepigwa na polisi
waliofyatua risasi za mipira kuutawanya umati wa wafuasi wake
akizungumza na mwandishi wa habari akiwa kitandani Hospitalini meya huyo
Erias Lukwago anasema alizilai baada ya gesi ya kutoa machozi ilipo
tupwa ndani ya gari lake.
Anaeleza kwamba maafisa wa polisi anasema walimpiga kifuani na kuzirarua
nguo zake waki mshutumu kwa kuchochea ghasia.Meya huyo ni mpenzani wa
rais wa nchini humu Yoweri Museveni.
Mtu mmoja anaripotiwa kufariki na wengine kadha kukamatwa wakati wa
ghasia hizo.Hatahivyo polisi wamekanusha madai ya kumpiga meya huyo
ambaye pia ni mkosaji mkubwa wa rais Museveni.
Upinzani unasema kuwa serikali inajaribu kukandamiza kilio cha mageuzi
nchini humo.Katika tukio jingine kiongozi wa upinzani Kizza Besigy
alikamatwa kwa kuandaa mkutano ambao polisi hawa kuidhinisha.
Bwana Lukwago jana alikuwa anaelekea kwenye jopo maalumu kwa mara ya
kwanza ambayo huenda ikamuondolea wadhifa wake kwa kosa la matumizi
mabaya ya ofisi.Mwandishi wa Habari Catherina Byaruhanga akiwa mjini
Kampala ana sema kuwa,Polisi walizingila nyumba yake na kisha kumpeleka
ambako jopo lilikuwa lina endesha vikao vyake.
Lakini akiwa anapelekwa polisi walirusha vikebe vya gesi ya kutoa
machozi ndani ya gari lake.Walinipiga kifuani na kudai na chochea ghasia
walinirarulia nguo zangu na kunitesa kwa kila njia nilijaribu kuwambia
wani ache lakini sikufanikiwa alisema Lukwago.
Kizza Besigye amedaiwa na polisi kuchochea umati wa watu mjini Kampala
ili kumuunga mkona bwa Lukwago kosa ambalo ofisi yake imekanusha.