Friday, November 15, 2013

MFANAYAKAZI WA TFF ATUMIA FULSA KWENYE MECHI YA AZAM NA MBEYA CITY KWA KUTENGENEZA TIKETI FEKI



  • Habari za uhakika ambazo Mwananchi imezipata kutoka ndani ya shirikisho hilo zimesema kuwa mfanyakazi huyo ametakiwa kutoa maelezo ya kutosha hadi ifikapo leo huku akitakiwa kutaja wahusika alioshirikiana nao kuhujumu mapato ya mchezo huo.
Mfanyakazi huyo ametakiwa kutoa maelezo ya kutosha hadi ifikapo leo.
Dar es Salaam. Mfanyakazi mmoja wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) amekamatwa na tiketi feki za mchezo wa Azam na Mbeya City uliofanyika wiki iliyopita na timu hizo kutoka sare ya mabao 3-3 mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Azam Complex.
Habari za uhakika ambazo Mwananchi imezipata kutoka ndani ya shirikisho hilo zimesema kuwa mfanyakazi huyo ametakiwa kutoa maelezo ya kutosha hadi ifikapo leo huku akitakiwa kutaja wahusika alioshirikiana nao kuhujumu mapato ya mchezo huo.
Chanzo kimedai kuwa mfanyakazi huyo amekuwa akishirikiana na vigogo wengine wa soka mtandao ambao umeota mizizi tangu uongozi uliopita wa TFF.
Sakata la mfanyakazi huyo liliibuka kwenye kikao cha Rais mpya wa TFF, Jamal Malinzi alipofanya mazungumzo na wafanyakazi wa shirikisho hilo akiwahakikishia kuboresha maslahi yao na kuwataka kufanya kazi kwa uhuru na amani na kuepuka kusikiliza maneno yanayoendelea hivi sasa huku baadhi yao wakiwa hawajui hatma ya ajira zao.
Hata hivyo Mwananchi ilipomtafuta Mkurugenzi wa Bodi ya Ligi, Silas Mwakibinga kuhusiana na suala hilo alisema “kuna mjumbe mmoja wa Kamati ya Utendaj alishtukia mchezo mchafu ambao mfanyakazi wa TFF anaucheza getini wakati wa mechi hiyo akamfukuza kukaa getini.
“Mbali na mfanyakazi huyo pia kuna watu wawili ambao walikamatwa na walilala kituo cha Polisi Mbagala baada ya kukutwa na vitabu viwili vya bei ya Sh 3,000. “Walichokuwa wanakifanya hawa mabwana ni kwamba tiketi moja inachanwa mara mbili na kuuziwa watu wawili tofauti kwa gharama ya sh 3000 kila moja.
Mwakibinga alidai watu hao wawili walikamatwa na walilala Polisi na kufunguliwa jalada lenye RB No. MBL/RB/11851/2013.
“Walighushi tiketi kitabu namba 07901 hadi 08000 kikiwa na tiketi mia na sikumbuki kitabu chake kilikuwa namba ngapi ili namba zake zilifuatana na hizo,” alisema.