
Jingine la kufahamu ni kwamba, Watalii wanaotembelea Tanzania kutoka nje ya nchi idadi yao imekua ikiongezeka kila mwaka kutoka Watalii laki nane na elfu 67,994 mwaka 2011 mpaka milioni moja na elfu sabini na saba 58 mwaka 2012.
Philiph Chitaunga ambae ni meneja wa huduma za utalii kutoka bodi ya utalii Tanzania amesema sasa hivi kuna mpango maalum kutangaza vivutio vya utalii vilivyoko Tanzania.