Saturday, October 12, 2013

SECTOR YA UTALII IMEONGEZEKA KWA 24% MPAKA KUFIKIA Tsh TRILIONI 2.69 KWA MWAKA 2012



Utalii 2Unaambiwa Utalii nchini Tanzania kwa mwaka 2012 peke yake umeingiza shilingi Trilioni 2.69 kwenye pato la taifa ikiwa ni ongezeko la asilimi 24 ikilinganishwa na mwaka 2011.
Jingine la kufahamu ni kwamba, Watalii wanaotembelea Tanzania kutoka nje ya nchi idadi yao imekua ikiongezeka kila mwaka kutoka Watalii laki nane na elfu 67,994 mwaka 2011 mpaka milioni moja na elfu sabini na saba 58 mwaka 2012.
Philiph Chitaunga ambae ni meneja wa huduma za utalii kutoka bodi ya utalii Tanzania amesema sasa hivi kuna mpango maalum kutangaza vivutio vya utalii vilivyoko Tanzania.