Wednesday, October 2, 2013

MATOKEO NA RATIBA YA UEFA CHAMPION LEAGUE

Michuano ya Ligi ya mabingwa barani Ulaya maarufu kama UEFA Champions league imeendelea usiku wa jana kwa michezo nane ikiwa ni sehemu ya kwanza ya raundi ya pili ya hatua ya makundi .
Klabu ya Arsenal iliendeleza mwanzo wake mzuri baada ya kuifunga Napoli kwa mabao mawili bila .
Arsenal ambao wako kundi F walifunga mabao yao kupitia kwa Mesut Ozil huku Olivier Giroud akifunga bao lingine .
uefa 1
Katika mchezo mwingine wa Kundi F Borrusia Dortmund waliwafunga Olympique Marseile kwa matokeo ya 3-0 . Marco Reus na Robert Lewandowski ndio waliofunga mabao ya Dortmund ambapo Lewandowski alifunga mabao mawili .
Matokeo hayo yanamaanisha kuwa Arsenal wanaongoza kundi hilo wakiwa wamekusanya pointi sita baada ya mechi mbili huku Napoli na Dortmund ambao wameshinda na kupoteza mechi moja moja wakiwa na pointi tatu na Marseile hawana pointi yoyote .
Katika michezo mingine Fc Barcelona waliwafunga Glasgow Celtic 1-0 bao pekee la mchezo huo likifungwa na Cesc Fabregas . Kwingineko Ajax Amsterdam na Ac Milan walitoka sare ya 1-1.
uefa 2
Fc Porto wakiwa nyumbani kwao walipoteza mchezo wao dhidi ya Atletico Madrid kwa matokeo ya 2-1 . Porto walianza kufunga kupitia kwa Jackson Martinez lakini Madrid walisawazisha kupitia kwa Arda Turan na Diego alifunga bao la ushindi .Mchezo mwingine wa kundi hilo hilo ulishuhudia Zenith St Petersburg na Austria Vienna wakitoka sare ya 1-1.
Huku jijini Bucharest Chelsea hawakuwa na Huruma mbele ya wenyeji wao Steau Bucuresti baada ya kuwafunga 0-4 . Wafungaji wa Chelsea katika mchezo huo walikuwa Ramires aliyefunga mabao mawili , Frank Lampard huku Mlinzi wa Bucuresti Daniel Georgievski akijifunga mwenyewe kwenye bao lingine .
uefa 3
Schalke 04 wakiwa ugenini nchini Uswisi waliwafunga Fc Basel 1-0 . Bao pekee la mchezo huo lilifungwa na Jullian Draxler .
Michuano hiyo itaendelea hii leo ambapo Manchester United watakuwa wageni wa Shakhtar Donetsk huko Ukraine , Real Sociedad watasafiri hadi nchini Ujerumani kucheza na Bayer Leverkusen , Real Madrid watawakaribisha Fc Copenhagen huku Juventus nao wakiwa wenyeji wa Galatasaray .
Michezo mingine itawashuhudia Manchester City wakicheza na mabingwa watetezi Bayern Munich , Viktoria Plzen nao wakicheza na CSKA Moscow pamoja na Paris St Germain dhidi ya Benfica na Anderletch wakicheza na Olympiakos.