
Mwandishi wa habari Denice Stephano anakwambia hii ishu imefanya wapatikane watuhumiwa tisa
wa kesi ya wizi wa mafuta katika mgodi wa Dhahabu ( GEITA GOLD MINE )
kwa kutumia gari la wagonjwa (Ambulance) ambapo wamefikishwa mahakamani
na kusomewa mashitaka matatu.
Mwendesha
mashitaka wa polisi Inspekta Abiner ameiambia mahakama September 9 2013
kwamba 5/09/2013 saa 7:30 usiku uko eneo la Geita power ndani ya mgodi
wa Geita gold mine watuhumiwa waliiba mafuta lita 630 ya dizeli, kula
njama za kuiba mafuta hayo na kuharibu mali ambayo ni gari la kubeba
wagojwa katika kituo cha Afya cha Nzera kwa kuling’oa viti
Mtuhumiwa wa kwanza Hamudi Biemo (28) Dereva wa gari anatuhumiwa makosa matatu likiwemo la kula njama na kung’oa viti vya gari.
Abiner
ameongeza kuwa washitakiwa hao walitumia gari aina ya Land Crusser
yenye namba za usajili T 671 AKW mali ya Halmashauri ya wilaya ya Geita na
kuingia mgodini kuiba mafuta aina ya Diesel lita 630 yenye thamani ya
Tsh. 1,386,000/= mali ya Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM)
Waliofikishwa
mahakamani ni Hamudi Biembo dereva wa gari la wagonjwa ,Malemo Paul
(31) mkazi wa mtaa wa Mseto Geita,Selemani Magoso (31 )ambaye ni
dereva pikipiki mkazi wa mtaa wa Shilabela Geita, Julias Boazi (28)
mkazi wa Msalala road Geita )Wengine ni Rashid
Hussen (27) Mlizi wa mgodi, Ismail Zuber (26)mlinzi wa Kampuni ya G4S
,Christoper Kombo Operator wa GGM,Joseph Chiristopher (27) Operator wa
GGM