Friday, June 28, 2013

SUGU HURU BAADA YA HATI YA MASHTAKA KUONESHA MAPUNGUFU


MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Dodoma Mjini, jana ilimuachia huru Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (41), maarufu kama Sugu aliyefikishwa mahakamani kwa kosa la kutumia lugha ya matusi dhidi ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda baada ya hati ya mashtaka kuonesha mapungufu.
Kutokana na uamuzi huo wa Mahakama imeutaka upande wa mashtaka kurekebisha hati hiyo na kumfikisha tena mshtakiwa mahakamani huku Wakili wa Mbilinyi, Tundu Lissu akitaka kesi mpya itakayoletwa mahakamani iwe na maelezo ya Waziri Mkuu na awe tayari kusimama mahakamani kuthibitisha shitaka hilo.
Kesi hiyo ilikuwa ikisikilizwa na Hakimu Mkazi Mfawidhi, Elinaza Luvanda.
Awali akimsomea mashtaka, Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Harriet Lopa alidai kuwa Juni 24, mwaka huu, Mbilinyi akiwa Dodoma alituma ujumbe wenye lugha ya matusi kwa kutumia mtandao wa kijamii wa Facebook kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Mshtakiwa alikana shitaka hilo. Hata hivyo wakili wa Mshtakiwa, Lissu aliomba kutoa hoja na kusema hati ya mashtaka ni mbovu na kuomba Mahakama itupilie mbali kwa sababu ina makosa.
“Lugha ya matusi haikutajwa, lugha gani hiyo ya matusi na hati ya mashtaka iko kimya, mshtakiwa atajitetea vipi,ataandaa utetezi namna gani kwani hata kinachodaiwa kuwekwa kwenye facebook hakijasemwa,” alidai Lissu.
Akijibu hoja hiyo, Wakili wa Serikali alisema kesi hiyo bado iko kwenye upelelezi na kutaka mshtakiwa aendelee na mashtaka yake mpaka itakapothibitishwa vinginevyo.
Kutokana na kauli hiyo ya wakili wa Serikali, Lissu alizidi kusisitiza hati ya mashtaka haina maelezo ya kutosha na inatakiwa kukidhi matakwa ya sheria.
“Hati ya mashtaka iliyoletwa si halali kinyume na kifungu cha 132 cha mwenendo wa makosa ya jinai na itakuwa makosa kama Mahakama ikikubali hati hiyo,” alisema.
Alitoa uamuzi wa Mahakama, Hakimu Luvanda alisema anakubaliana na maelezo ya Wakili upande wa utetezi Lissu kuwa hati hiyo ina mapungufu.
Alisema Mahakama inamuachia huru mshtakiwa na upande wa mashtaka unaweza kumshtaki tena mshtakiwa kama itaona umuhimu wa kufanya hivyo.
Akizungumza nje ya Mahakama Lissu alisema hati ya mashtaka dhidi ya Mbilinyi kuwa alitoa lugha ya matusi kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda haijaeleza anachodaiwa kusema Mbilinyi.
Alisema Mahakama imetenda sawasawa kuifuta hati hiyo ilitakiwa ifafanue lugha ya matusi iliyotumika ni ipi. ”Hakimu hajasema Sugu hana makosa, lakini upande wa mashtaka ukajipange kutengeneza hati mpya,” alisema.

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Dodoma imetupilia mbali mashitaka yaliyokuwa yamefunguliwa na serikali dhidi ya Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (CHADEMA) kwa madai ya kumtukana Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Akitoa hukumu hiyo, Hakimu Mfawidhi wa mahakama hiyo, Eliezel Luvanda alitupilia mbali mashitaka hayo kutokana na hati ya mashitaka dhidi ya mbunge huyo kuwa na upungufu.
Luvanda alisema kwa mujibu wa kifungu cha sheria cha 132 (20) hati hiyo haikuwa na maelezo ya kutosheleza kuonesha ni lugha gani iliyodaiwa kuwa ni ya matusi aliyotumia mshitakiwa huyo dhidi ya Pinda.
Awali akisoma hati hiyo, Mwendesha Mashitaka, Hariet Lopa alidai kuwa Juni 24 mwaka huu akiwa katika Manispaa ya Dodoma, Mbilinyi aliweka ujumbe wenye lugha ya matusi dhidi ya Waziri Mkuu Pinda kinyume cha sheria.
Kabla ya hakimu kutoa hukumu hiyo, wakili na mwanasheria wa CHADEMA, Tundu Lisu, aliwasilisha utetezi wake mbele ya mahakama hiyo akiitaka kuitupilia mbali kesi hiyo kwa vile hakuna matusi yanayotajwa yakidaiwa kutolewa na mbunge huyo dhidi ya Pinda.
Lissu alisema kuwa kwa mujibu wa kifungu cha sheria cha 132 (20), hati hiyo haikuwa na maelezo ya kutosheleza kuonesha ni lugha gani iliyotumika na ni matusi gani, hivyo haiwezi kuwa kesi ambayo inaweza kuendelea kusikilizwa.
Lissu alidai kuwa maneno yanayodaiwa yangesababisha uvunjifu wa amani hayakutajwa katika hati hiyo huku akihoji upande wa mashitaka unataka Sugu ajitetee kwa shitaka lipi.
Aliendelea kuieleza mahakama hiyo kuwa kama hati hiyo ya mashitaka iliyopelekwa mahakamani hapo itaendelea kutumika, itakuwa imekiuka sheria, hivyo akaitaka mahakama hiyo kuifuta kesi hiyo.
Hakimu Luvanda alipomtaka mwendesha mashitaka wa serikali kujibu hoja ya Lissu, alishikilia msimamo wake na kuiomba mahakama kuendelea kuisikiliza kesi hiyo kwa madai kuwa ni mpya, hivyo makosa ambayo yapo yatafanyiwa marekebisho wakati shauri likiendelea.
Hata hivyo Lissu alipinga kauli ya mwanasheria wa serikali kwa madai kuwa hati ya mashitaka ni chafu na imeandaliwa ovyo, hivyo mahakama kukubali kuendelea kusikiliza kesi hiyo ni kosa na hivyo ni vyema ikatupiliwa mbali.
“Mheshimiwa hakimu naomba kesi hii itupiliwe mbali kwa kuwa hati ya mashitaka ni chafu na ni ya ovyo. Naomba itupiliwe mbali na mtuhumiwa aachiwe huru,” alisema Lissu na kuongeza kuwa wapo tayari hata kesho kuendelea na kesi hiyo ikiwa serikali itaandaa hati sahihi.
Hata hivyo, baada ya hakimu huyo kutoa hukumu hiyo, mwendesha mashitaka alidai wataendelea na upelelezi na ukikamilika wataandaa hati mpya.
Akizungumza mara baada ya hukumu hiyo, Lissu alisema mahakama hiyo imetenda haki na kama upande wa mashitaka haukuwa umeridhika na hukumu hiyo, ujipange upya na kupeleka hati ya mashitaka.
Lissu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA) alisema hata hivyo kufutwa kwa kesi hiyo hakumaanishi mteja wake hawezi kushitakiwa tena, kwani bado Waziri Mkuu Pinda anaweza kwenda polisi kutoa maelezo kama anaona kweli ametendewa kosa hilo.
Kwa upande wake, Sugu baada ya kuachiwa huru alisema kuwa anachoshauri ni Pinda kujitafakari upya juu ya kauli zake anazozitoa hasa kuhamasisha watu kupigwa.
Awali, Sugu alikamatwa na Jeshi la Polisi mkoani hapa kwa tuhuma kuwa aliweka ujumbe mfupi katika mtandao wa kijamii ambao ulikuwa unamtusi Waziri Mkuu Pinda.
Hata hivyo, alikuwa akipelekwa katika kituo cha polisi cha kati kwa mahojiano na jana ilikuwa ni mara ya kwanza kufikishwa mahakamani
- See more at: http://kariakoodsm.blogspot.com/2013/06/sugu-ambwaga-pinda.html#sthash.LeAiO4F8.bnKoc1Do.dpuf

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Dodoma imetupilia mbali mashitaka yaliyokuwa yamefunguliwa na serikali dhidi ya Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (CHADEMA) kwa madai ya kumtukana Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Akitoa hukumu hiyo, Hakimu Mfawidhi wa mahakama hiyo, Eliezel Luvanda alitupilia mbali mashitaka hayo kutokana na hati ya mashitaka dhidi ya mbunge huyo kuwa na upungufu.
Luvanda alisema kwa mujibu wa kifungu cha sheria cha 132 (20) hati hiyo haikuwa na maelezo ya kutosheleza kuonesha ni lugha gani iliyodaiwa kuwa ni ya matusi aliyotumia mshitakiwa huyo dhidi ya Pinda.
Awali akisoma hati hiyo, Mwendesha Mashitaka, Hariet Lopa alidai kuwa Juni 24 mwaka huu akiwa katika Manispaa ya Dodoma, Mbilinyi aliweka ujumbe wenye lugha ya matusi dhidi ya Waziri Mkuu Pinda kinyume cha sheria.
Kabla ya hakimu kutoa hukumu hiyo, wakili na mwanasheria wa CHADEMA, Tundu Lisu, aliwasilisha utetezi wake mbele ya mahakama hiyo akiitaka kuitupilia mbali kesi hiyo kwa vile hakuna matusi yanayotajwa yakidaiwa kutolewa na mbunge huyo dhidi ya Pinda.
Lissu alisema kuwa kwa mujibu wa kifungu cha sheria cha 132 (20), hati hiyo haikuwa na maelezo ya kutosheleza kuonesha ni lugha gani iliyotumika na ni matusi gani, hivyo haiwezi kuwa kesi ambayo inaweza kuendelea kusikilizwa.
Lissu alidai kuwa maneno yanayodaiwa yangesababisha uvunjifu wa amani hayakutajwa katika hati hiyo huku akihoji upande wa mashitaka unataka Sugu ajitetee kwa shitaka lipi.
Aliendelea kuieleza mahakama hiyo kuwa kama hati hiyo ya mashitaka iliyopelekwa mahakamani hapo itaendelea kutumika, itakuwa imekiuka sheria, hivyo akaitaka mahakama hiyo kuifuta kesi hiyo.
Hakimu Luvanda alipomtaka mwendesha mashitaka wa serikali kujibu hoja ya Lissu, alishikilia msimamo wake na kuiomba mahakama kuendelea kuisikiliza kesi hiyo kwa madai kuwa ni mpya, hivyo makosa ambayo yapo yatafanyiwa marekebisho wakati shauri likiendelea.
Hata hivyo Lissu alipinga kauli ya mwanasheria wa serikali kwa madai kuwa hati ya mashitaka ni chafu na imeandaliwa ovyo, hivyo mahakama kukubali kuendelea kusikiliza kesi hiyo ni kosa na hivyo ni vyema ikatupiliwa mbali.
“Mheshimiwa hakimu naomba kesi hii itupiliwe mbali kwa kuwa hati ya mashitaka ni chafu na ni ya ovyo. Naomba itupiliwe mbali na mtuhumiwa aachiwe huru,” alisema Lissu na kuongeza kuwa wapo tayari hata kesho kuendelea na kesi hiyo ikiwa serikali itaandaa hati sahihi.
Hata hivyo, baada ya hakimu huyo kutoa hukumu hiyo, mwendesha mashitaka alidai wataendelea na upelelezi na ukikamilika wataandaa hati mpya.
Akizungumza mara baada ya hukumu hiyo, Lissu alisema mahakama hiyo imetenda haki na kama upande wa mashitaka haukuwa umeridhika na hukumu hiyo, ujipange upya na kupeleka hati ya mashitaka.
Lissu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA) alisema hata hivyo kufutwa kwa kesi hiyo hakumaanishi mteja wake hawezi kushitakiwa tena, kwani bado Waziri Mkuu Pinda anaweza kwenda polisi kutoa maelezo kama anaona kweli ametendewa kosa hilo.
Kwa upande wake, Sugu baada ya kuachiwa huru alisema kuwa anachoshauri ni Pinda kujitafakari upya juu ya kauli zake anazozitoa hasa kuhamasisha watu kupigwa.
Awali, Sugu alikamatwa na Jeshi la Polisi mkoani hapa kwa tuhuma kuwa aliweka ujumbe mfupi katika mtandao wa kijamii ambao ulikuwa unamtusi Waziri Mkuu Pinda.
Hata hivyo, alikuwa akipelekwa katika kituo cha polisi cha kati kwa mahojiano na jana ilikuwa ni mara ya kwanza kufikishwa mahakamani
- See more at: http://kariakoodsm.blogspot.com/2013/06/sugu-ambwaga-pinda.html#sthash.LeAiO4F8.bnKoc1Do.dpuf

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Dodoma imetupilia mbali mashitaka yaliyokuwa yamefunguliwa na serikali dhidi ya Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (CHADEMA) kwa madai ya kumtukana Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Akitoa hukumu hiyo, Hakimu Mfawidhi wa mahakama hiyo, Eliezel Luvanda alitupilia mbali mashitaka hayo kutokana na hati ya mashitaka dhidi ya mbunge huyo kuwa na upungufu.
Luvanda alisema kwa mujibu wa kifungu cha sheria cha 132 (20) hati hiyo haikuwa na maelezo ya kutosheleza kuonesha ni lugha gani iliyodaiwa kuwa ni ya matusi aliyotumia mshitakiwa huyo dhidi ya Pinda.
Awali akisoma hati hiyo, Mwendesha Mashitaka, Hariet Lopa alidai kuwa Juni 24 mwaka huu akiwa katika Manispaa ya Dodoma, Mbilinyi aliweka ujumbe wenye lugha ya matusi dhidi ya Waziri Mkuu Pinda kinyume cha sheria.
Kabla ya hakimu kutoa hukumu hiyo, wakili na mwanasheria wa CHADEMA, Tundu Lisu, aliwasilisha utetezi wake mbele ya mahakama hiyo akiitaka kuitupilia mbali kesi hiyo kwa vile hakuna matusi yanayotajwa yakidaiwa kutolewa na mbunge huyo dhidi ya Pinda.
Lissu alisema kuwa kwa mujibu wa kifungu cha sheria cha 132 (20), hati hiyo haikuwa na maelezo ya kutosheleza kuonesha ni lugha gani iliyotumika na ni matusi gani, hivyo haiwezi kuwa kesi ambayo inaweza kuendelea kusikilizwa.
Lissu alidai kuwa maneno yanayodaiwa yangesababisha uvunjifu wa amani hayakutajwa katika hati hiyo huku akihoji upande wa mashitaka unataka Sugu ajitetee kwa shitaka lipi.
Aliendelea kuieleza mahakama hiyo kuwa kama hati hiyo ya mashitaka iliyopelekwa mahakamani hapo itaendelea kutumika, itakuwa imekiuka sheria, hivyo akaitaka mahakama hiyo kuifuta kesi hiyo.
Hakimu Luvanda alipomtaka mwendesha mashitaka wa serikali kujibu hoja ya Lissu, alishikilia msimamo wake na kuiomba mahakama kuendelea kuisikiliza kesi hiyo kwa madai kuwa ni mpya, hivyo makosa ambayo yapo yatafanyiwa marekebisho wakati shauri likiendelea.
Hata hivyo Lissu alipinga kauli ya mwanasheria wa serikali kwa madai kuwa hati ya mashitaka ni chafu na imeandaliwa ovyo, hivyo mahakama kukubali kuendelea kusikiliza kesi hiyo ni kosa na hivyo ni vyema ikatupiliwa mbali.
“Mheshimiwa hakimu naomba kesi hii itupiliwe mbali kwa kuwa hati ya mashitaka ni chafu na ni ya ovyo. Naomba itupiliwe mbali na mtuhumiwa aachiwe huru,” alisema Lissu na kuongeza kuwa wapo tayari hata kesho kuendelea na kesi hiyo ikiwa serikali itaandaa hati sahihi.
Hata hivyo, baada ya hakimu huyo kutoa hukumu hiyo, mwendesha mashitaka alidai wataendelea na upelelezi na ukikamilika wataandaa hati mpya.
Akizungumza mara baada ya hukumu hiyo, Lissu alisema mahakama hiyo imetenda haki na kama upande wa mashitaka haukuwa umeridhika na hukumu hiyo, ujipange upya na kupeleka hati ya mashitaka.
Lissu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA) alisema hata hivyo kufutwa kwa kesi hiyo hakumaanishi mteja wake hawezi kushitakiwa tena, kwani bado Waziri Mkuu Pinda anaweza kwenda polisi kutoa maelezo kama anaona kweli ametendewa kosa hilo.
Kwa upande wake, Sugu baada ya kuachiwa huru alisema kuwa anachoshauri ni Pinda kujitafakari upya juu ya kauli zake anazozitoa hasa kuhamasisha watu kupigwa.
Awali, Sugu alikamatwa na Jeshi la Polisi mkoani hapa kwa tuhuma kuwa aliweka ujumbe mfupi katika mtandao wa kijamii ambao ulikuwa unamtusi Waziri Mkuu Pinda.
Hata hivyo, alikuwa akipelekwa katika kituo cha polisi cha kati kwa mahojiano na jana ilikuwa ni mara ya kwanza kufikishwa mahakamani
- See more at: http://kariakoodsm.blogspot.com/2013/06/sugu-ambwaga-pinda.html#sthash.LeAiO4F8.bnKoc1Do.dpuf